Wednesday 7 May 2014

Sentensi 12 alizozitoa ktk bunge la katiba Mh. Joseph Mbilinyi (Sugu) leo na sauti yake.


BUNGENI DODOMA TANZANIA KWENYE VIKAO VINAVYOENDELEA

 
Wajumbe mbalimbali kwenye bunge la katiba wameendelea kuwasha vipaza sauti vyao kuchangia, kutoa ya moyoni kwa kujadili sura ya kwanza na ya sita huku ishu ya serikali mbili au tatu ikizimiliki headlines zaidi.

Zifuatazo ni kauli za mjumbe Mh. Joseph Mbilinyi ambae pia ni mbunge wa Mbeya mjini April 15 2014
1. ‘Wabunge Wakristo hii ni kwaresma, ni kipindi cha toba… mnatumia kipindi hiki kufanya unafiki mbele ya Wananchi mtakuja kuhukumiwa siku itakapofika, wameharibu mchakato wakati tumeshatumia mabilioni mengi ya hela’
2. ‘Ukarabati tu wa jengo la bunge hili ili sisi tukae zimetumika BILIONI 8.2 alafu leo kwa sababu ya hotuba moja tu ya Mwenyekiti wa chama cha mapinduzi wote wamegeuka, wanaharibu kabisa tunashindwa kufanya mambo ya maana, wanaacha kupanga mkakati wa hoja wanapanga mkakati wa kuzomea, wameishiwa mikakati mpaka wanazomea kimkakati’
3. ‘Unakutana na mbunge tena Waziri kama rafiki yangu Mwigulu Nchemba tunataniana ananiita mzee wa Maandamano mi namuita mzee wa kuteka, ananiambia wewe Sugu sijui unataka serikali tatu sijui vipi na vipi, namwambia kwani hutaki kabisa Tanganyika anasema mi nataka Tanganyika ila nataka serikali moja, sasa kama mnataka serikali moja kwa nini uibuke kwenye hoja ya serikali mbili?
4. ‘Kuna watu ambao wanajadili vitu ambavyo hawaviamini na havipo kwenye mioyo yao na hao watu wanadhamana kwenye uongozi wa taifa hili na hii ni hatari

 
5.  ‘Tuko kwenye nafasi nzuri sana ya kujadili hili swala, tulijadili wakati tunaheshimiana kuliko siku tuje kulazimisha mabadiliko ambayo hatukuyapanga, tusifikie sehemu Wazanzibari hao wanaosemwa elfu sitini ndio waingie barabarani na jeshi’

6. ‘Mwenyekiti alikuja hapa akatutisha oooh sijui serikali tatu jeshi, Mwanajeshi atakuja atachukua nchi… Mwenyekiti mwenyewe alikua ni Mwanajeshi akavua uniform, Nyerere aliposema vueni uniform akavua na leo ni rais, kuna ubaya gani Mwanajeshi akitawala kama ana akili? hakuna ubaya, wanajeshi ni ndugu zetu’
7. ‘Hakuna tatizo lolote siku Mwanajeshi akija kuwa Rais kwa sababu tunae Mwanajeshi Rais Kikwete na anaendelea tu, asiweke vikwazo kwa Wanajeshi wengine ambao watakua na tija kwa taifa hili’
8. ‘Wanasema serikali tatu gharama, hivi kama gharama inaongezeka alafu tija inaongezeka kuna tatizo gani? ukifanya biashara rejareja ukitaka kuwa mkubwa ni lazima uongeze mtaji, kama huu mfumo wa serikali mbili umeshindwa kutuondolea matatizo mwengine anasema Znz wana hiki wana kile, mbona hamsemi kama mpaka umeme tunawalipia?? lakini sisi huku tunalia
‘Tuna serikali mbili na hakuna aliesimama hapa akasema serikali mbili gharama zake zipi, Wizara ngapi hapa zinapanga  majengo kila siku yanatolewa furniture? serikali tatu gharama against what? against tija? against maendeleo? against kwenda mbele? 10. ‘Sababu akili yenu ni fedha ndio maana mnaangalia faida kwamba ni fedha tu, hamuangalii faida nyingine za kijamii ambazo zitaleta tija kwa taifa hili’
11. ‘Kuna hawa ndugu zangu viongozi wa dini, tunasema hivi mara nyingi viongozi wa dini wamekosea walipochagua kuwa upande wa dola dhidi ya matakwa ya nchi, hii imetokea mfano ni Padri wa Rwanda, leo hii yukwapi? kwa hiyo viongozi wa dini wawe makini wanavyoangazia haya maswala’
12. ‘Mungu ibariki Tanganyika, Mungu ibariki Zanzibar , Mungu bariki mchakato huu wa shirikisho la Zanzibar na Tanganyika, acheni kutupiga mkwara eti tutagawana mbao… ni heri kugawana mbao kuliko kwenda kuzinguana huko mbele ya safari

No comments:

Post a Comment